Thursday, May 24, 2012

PSI YATOA SEMINA YA KUJIKINGA NA MAAMBUKIZI YA UKIMWI KATIKA MABAA NA VILABU YA POMBE JIJINI MBEYA

SHIRIKA lisilo la kiserikali linalotoa huduma na Elimu ya Afya nchini(PSI) limeendelea kutoa huduma katika mabaa na vilabu vya pombe za kienyeji mmoja wa  waendesha semina Bi Anisa. akitoa maelekezo ya uvaaji wa kondom katika baa ya Blue house jijini Mbeya

Mmoja wa waliyopata semina hiyo ya maambukizi ya ukimwi Bwana Frumency  John kushoto  akijaribu kujibu swali aliloulizwa  na mtoa semina

Wednesday, May 23, 2012

UCHAMBUZI WA KILIMO CHA TUMBAKU



Habari na Ester Macha, Chunya.
Zao la Tumbaku ni zao ambalo limekuwa likiwakomboa wananchi na hivyo kupunguza ukali wa maisha waliyonayo hasa maeneo ya vijijini ambako wananchi wake wamekuwa na maisha magumu,licha ya kuwakomboa wananchi pia hata serikali imekuwa ikiongeza mapato yake kupitia halmashauri zake za wilaya zinazolima zao hilo.


Kilimo hicho cha Tumbaku kimekuwa kiingizia serikali dola za kimarekani 614.8 kutokana na ushuru unaotolewa baada ya mauzo ya zao hilo kwa wakulima.


Kwa kutambua hilo serikali imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha vyama vya ushirika ambavyo vimeundwa kwa lengo la kuwasaidia wakulima vinaboreshwa na hata kusaidia ili viweze kupata mikopo kutoka kwenye taasisi mbalimbali za kifedha lengo likiwa ni kumsaidia mkulima ili aboreshe kilimo cha tumbaku.


Vile vile hata ukiangalia katika halmashauri za Wilaya nchini ambazo zinalima tumbaku katika mapato yao ya halmashauri asilimia kubwa wamekuwa wakipata mapato makubwa kutokana na kilimo cha zao hilo na ndio kimekuwa mkombozi kwao.


Hata hivyo kilimo hicho kwa muda mrefu kimekuwa mkombozi kwa wakulima na hivyo kumwondolea umasikini  na hata halmashauri za Wilaya nchini ambazo mikoa yake inalima Tumbaku zimekuwa zinaongeza kipato kutokana na uuzaji wa Tumbaku ambapo kwa miaka miwili mfululizo zaidi ya sh.Bil.26 zimepatikana.


Hivi karibuni  Chama kikuu Cha Ushirika cha Wakulima wa Tumbaku Wilayani Chunya (CHUTCU LTD) kilifanya mkutano mkuu wa kawaida  na kuhudhuliwa na wanachama  wa vyama vya ushirika vya Msingi 21(AMCOS) ambavyo vinalima zao la Tumbaku  kupitia wanachama wake wa vyama vya ushirika vyenye wakulima zaidi ya 8,057.


Akizungumza  kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya katika mkutano huo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya Bi. Mariamu Mtunguja anasema kuwa mkutano huo uwe  na manufaa na ambao utalenga kujadili na kujenga ushirikiano na kukuza zao la tumbaku ambalo ni kichocheo cha maendeleo kwa wakulima.


Bi. Mtunguja anasema kuwa ili vyama vya ushirika viweze kuwa imara hakuna budi viongozi wanaopata madaraka kuhakikisha kuwa wanatatua matatizo ya wakulima ambao wamekuwa na matatizo mbalimbali katika kilimo cha Tumbaku hususani maeneo ya vijijini.


"Ndugu zangu viongozi hakikisheni mnafanya kazi vizuri ili kuondoa maswali kwa wakulima wenu kuwa mlipokuwa madarakani mlifanya nini, badala ya kiongozi kuhoji ushirika umemfanyia nini alipokuwa madarakani "alifafanua kiongozi huyo.


Hata hivyo Katibu Tawala huyo aliwataka wanaushirika kuwa mfano mzuri wa  kuigwa na wengine kwa kuondoa migogoro iliyopo ndani ya ushirika badala  yake wafanikishe maendeleo  mazuri kwa  wakulima waliowachagua na kwamba hiyo itawafanya waliowachagua wawe na imani na uongozi uliopo madarakani.


Akizungumzia kuhusu takwimu za uzalishaji wa zao hilo Kiwilaya Bi.Mtunguja anasema kuwa mekuwa ukipanda  kutoka tani 5,361 kwa msimu wa mwaka 2008/2009 hadi tani tani 7,540 kwa msimu wa mwaka 2009/2010 ikiwa ni ongozeko la zaidi ya asilimia 28.9 huku msimu wa mwaka 2010/2011 kukiwa na tani 12,570 zilizalishwa ambayo ni sawa na ongozeko la asilimia 40.21.


Hata hivyo Katibu Tawala huyo anasema kuwa kuongozeka kwa uzalishaji huo kumechangiwa na wanaushirika kuanza kujitegemea na hivyo kurudisha tija kwa wakulima kutokana na bei ya pembejeo inayotolewa bila faida ambazo zilikuwa zinawekwa na makampuni wakati wao wakiwa wanafanya biashara ya tumbaku


Aidha anaongeza kuwa  bei nzuri ya Tumbaku iliyotolewa kwa msimu wa mwaka 2008/2009/2010 ambayo  ilitokana na utaratibu wa wakulima kupitia vyombo vyao vya ushirika  kuagiza na kusambaza pembejeo kumejenga imani  kubwa na makampuni kuamini kuwa wanaushirika wanaweza wakiamua kwa umoja wao.




Anasema kuwa  pia mfumo huo unaweza kupunguza kasi ya ongozeko la gharama za kilimo cha tumbaku hasa pembejeo za kilimo ambazo zimekuwa shida kwa wakulima.




Hata hivyo Katibu Tawala huyo anasema kuwa kutokana na kuthamini wakulima wake serikali itaendelea kuunga mkono kwa kuvidhamini vyama vya ushirika kupata mikopo kutoka katika mabenki mbalimbali ili waweze kuboresha kilimo cha tumbaku.


Kuhusu kudangwanywa wakulima Bi. Mtunguja aliwataka wakulima kuacha kudanganywa na watu wasiopenda  maendeleo ya ushirika kwa kuwaambia pembejeo zinatolewa na wanaushirika  kwa bei  kubwa na hazijakidhi


viwango na kusema kuwa yote ni kutaka kuwakatisha tamaa ili warudi kwenye shida walizokimbia.


Aidha Bi. Mtunguja anasema kuwa licha ya kuwa na ongozeko hilo la uzalishaji wa tumbaku la zaidi ya asimilia 100 bado bei ya tumbaku ilishuka kutoka wastani wa USD 2.34 kwa kilo katika msimu wa mwaka 2010/2011 hadi kufikia wastani wa dola 1.4 kwa tumbaku ya mvuke katika msimu wa kilimo uliopita.


Anasema kuwa hata baada ya  mahitaji kuongozeka kimataifa tumbaku ilihitajika tena kwa wingi na ndio maana msimu ujao wa mauzo  bei ya msingi ya Tumbaku ya mvuke imepanda kufikia dola za kimarekani 1.82 kwa kilo na bado kuna makampuni yamelata mahitaji mengine.


Aidha Katibu Tawala huyo amewataka wakulima wa tumbaku kulima mazao mbadala kutokana na zao hilo kuendelea kupigwa vita na wanaharakati mbalimbali duniani.


Anasema kuwa licha ya kuwa zao hilo bado linaendelea kupigwa vita lakini ni vema wakulima  pia wakajikita zaidi na mazao mengine ambayo yanakubali katika maeneo hayo ambayo nayo yatakuwa mkombozi kwa mkulima.




Bi. Mtunguja anasema kuwa kauli hiyo hailengi kukataza kilimo cha zao hilo bali kuanza kuchukua tahadhari  mapema kwakuwa hakuna ajuaye nini yatakuwa matokeo ya hoja zinazojadiliwa na kupiganiwa na wanaharakati wanaopinga uvutaji wa sigara.




Aliyataja mazao yanayoweza kupewa nafasi na kuleta manufaa makubwa kwa wakulima kuwa ni pamoja na ufuta unaostawi katika ardhi ya wilaya ya Chunya, karanga pamoja na alizeti.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa CHUTCU Wilaya ya Chunya Bw. Sebastian Mogela amekiri ushirika kuendelea  yategemea makampuni ni kuchelewa kupiga hatua kimaendeleo akisema yapo kwaajili ya kufanya biashara yapate faida na si kutoa misaada kwa wakulima.






Bw.Mogela amesisitiza kuwa za umuhimu wa chama kikuu hicho kuwa na maofisa ugani wake ili waweze kusimamia kwa karibu kilimo hicho na kuleta manufaa zaidi kwa wakulima badala ya kuendelea kutumia wataalamu wa makampuni yanayonunua tumbaku.






Anasema kuwa hiyo itasaidia wakulima kupatiwa ushauri kupitia maafisa wao kuliko kutumia makampuni binafsi anayonunua tumbaku.


Hata hivyo kwa kutambua umuhimu wa zao la tumbaku bodi  ya Tumbaku nchini  hivi karibuni ilifanya mkutano wake maalamu ambao lengo lake kuu ilikuwa ni kujadili kupandisha kiwango cha uzalishaji kutoka tani 50,000 mwaka 2009 hadi kufikia tani 100,000 kwa mwaka 2010 jambo ambalo lilifikiwa kwa kuzalisha tani 126 sawa na asilimia 103.


Akizungumza katika huo maalamu Mwenyekiti wa Bodi ya Tumbaku Tanzania Vita Kawawa anasema kuwa pia lengo kubwa ya mkutano huo pia ni kuangalia changamoto za zao hilo na  na mafanikio


Anasema halmashauri za Wilaya nchini  pia zinaongeza kipato kutokana na uuzaji wa Tumbaku ambapo kwa miaka miwili mfululizo zaidi ya shilingi bilioni 26 zimepatikana.


Pia Bw. Kawawa anasema kuwa  mkutano huo uelekeze nguvu zake kuwakomboa wananchi wa Mkoa huo jinsi ya kufaidika kwa kupata ajira kutokana na kiwanda cha kusindika Tumbaku ambacho mpaka sasa kimekaa bila kufanya kazi zaidi ya miaka 10.


Hata hivyo Meneja Mkuu wa CHUTCU Wilayani Chunya Bw.. Bakari Kassia ametaja mikoa ambayo inalima tumbaku kuwa ni Mbeya, Shinyanga, Ruvuma, Iringa,Tabora, Rukwa mkoa wa katavi,Singida na Kigoma.


Anasema kuwa katika mikoa hiyo nane ndo imekuwa ikizalisha tumbaku kwa wingi na kwamba kwa Mkoa wa Mbeya ni Wilaya ya Chunya ambayo inalima kwa Tarafa tatu ambazo ni Kiwanja, Kwimba na Kipembawe.


Hata hivyo anasema kumekuwepo na changamoto mbali mbali katika halmashauri ya wilaya ya Chunya kushindwa kuwahimiza wananchi kuhusu kilimo cha tumbaku  wakati ndo kinaongoza kuwapatia mapato, kingine ni maafisa ushirika kushindwa kuhimiza wananchi kutokana na halmashauri kushindwa kuwapatia mahitaji muhimu ili waweze kuwahimiza wananchi.

KAMPENI ZA UCHAGUZI CHUO KIKUU CHA TEOFILO KISANJI (TEKU) ZAZINDULIWA RASMI.





Habari na Ezekiel Kamanga.
Wanawake wawili wajitokeza kugombea nafasi ya Urais na Makamu Rais.

Kampeni za uchaguzi wa 
kumpata Rais wa Chuo kikuu cha Teku, zimezinduliwa rasmi jana katika 
ukumbi wa Mwasakafyuka huku wagombea wakinadi sera zao.




Kampeni hizo zilizinduliwa
na Dakta Mozes D, na kusimamiwa na mkufunzi wa chuo Bwana Alawi 
Mikidadi ambapo Mkurugenzi wa uchaguzi Bi Nyemba Joyce aliweka hadharani
wagombea watakao wania viti vya urais na makamu rais.




Majina hayo upande wa rais
ni Bi Somi Irene, Bwana George Godbless na Joshua Jason na upande wa 
Makamu ni Bi Wilson Gwantwa, Bwana Yohanna Yesse na Deus Petro.


Mwenyekiti wa tume ya 
uchaguzi Bwana Kavenga Emmanuel amesema kwamba mchakato wa uchaguzi 
ulianza Mei 9 mwaka ahuu kwa kujaza fomu ambapo wanachuo 70 walijitokeza
kuomba nafasi mbalimbali.




Aidha Mei
19 na 20 wagombea walifanyiwa wagombea usaili na kwamba majina 
yaliyotajwa hapo juu ndio yaliyopitishwa na tume hiyo na kwamba kampeni 
zimeanza rasmi jana ambazo zitaendelea mpaka Mei 28 asubuhi na uchaguzi 
utafanyika Mei 29 mwaka huu na matokeo yatatangazwa mei 30 mwaka huu na 
viongozi wote Rais na baraza la mawaziri kuapishwa Juni mosi mwaka huu.




Mwenyekiti huyo Bwana 
Kavenga amewataka viongozi hao kufanya kampeni za amani bila matusi 
kwani kampeni kwa kufanya hivyo haitawasaidia kupata kura, bali 
itawashushua heshima zao.


Kwa upande wake Rais 
anayemaliza muda wake Bwana Ambukege Imani ameishukuru tume ya uchaguzi 
kwa mchakato mzima na anafurahi kumaliza muda wake chuo kikiwa na amani 
na kuwataka watakaopata nafasi za kuongoza wazingatie sheria, demokrasia
na upendo ili kuleta mshikamano katika chuo, ili wanaoongozwa wajisikie
kuwa na amani kuwepo chuoni hapo badala ya kutatua migogoro isiyokuwa 
na maana.

Baadhi ya wabunge walipita bila kupingwa, kutokana na baadhi ya maeneo waliyokuwa wakiyagombea kutokuwa na wapinzani.


Hata
hivyo kujitokeza kwa wanawake kumeleta msisimko wa uchaguzi huo huku 
wanawake wakitoa majigambo kuwa wanawake wanaweza hata pasipo kuwezeshwa
na kwamba chuo hicho hakijawahi kupata viongozi wa juu ambao ni 
wanawake na kwamba imefika zamu yao kuongoza.

Monday, May 21, 2012

WASICHANA WA SHULE YA SEKONDARI MANYUNYU NJOMBE WAFAIDIKA NA SEMINA YA KUTUMIA KOPYUTA NA UMUHIMU WA MFUMO WA DIGITAL

Wasichana wa shule ya sekondari ya wasichana manyunyu mkoani njombe wakimsikiliza mwana sayansi wa masafa
Peter Kihogo kutoka mamlaka ya mawasiliano kanda ya nyanda za juu kusini

Mwanasayansi wa masafa Peter Kihogo akiendelea kuwaelimisha wasichana wa shule ya sekondari manyunyu juu ya umuhimu wa mawasiliano na faida zake katika masomo na shughuli mbalimbali za kila siku katika jamii

Katibu muhtasi mamlaka ya mawasiliano kanda ya nyanda za juu kusini Frida Msese akipeana ushauri na wasichana wa shule ya sekondari manyunyu

Wanafuzi wakiwa makini kumsikiliza mwanasayansi wa masafa


Mkuu wa shule ya ya sekondari manyunyu  Adolphina Katembo akiwashukuru waedesha semina ya mawasiliano na habari jamii toka mamalaka ya mawasiliano kanda ya nyada za juu kusini kuichagua shule yao kuwa mojawapo ya shule katika kupewa semina hiyo ya mawasiliano duniani

Sunday, May 20, 2012

Roma, Kiba, Dimpoz,AT, Suma Lee, Ben Pol, Barnaba wafunika Tamasha la Kili Winners Tour Mbeya usiku huu

 

 Roma Mkatoliki akitumbuiza jukwaani wakati wa show maalum ya Washindi wa Kili Music Awardjijini Mbeya katika Uwanja wa Sokoine jana.Picha zote na Father Kidevu Blog
 Suma Lee nae alishambulia jukwaa vilivyo na kuleta raha kwa mashabiki katika wakati wa show maalum ya Washindi wa Kili Music jijini Mbeya
 Ben Paul nae alishambulia jukwaa vilivyo na kuletya raha kwa mashabiki katika wakati wa show maalum ya Washindi wa Kili Music Award jijini Mbeya.
 Barnaba Boy ambaye ni mshindi wa Tuzo ya Mwimbaji Bora wa Kiume akimbo jukwaani hii leo wakati wa show maalum ya Washindi wa Kili Music Award jijini Mbeya katika Uwanja wa Sokoine
 Vijana wengi walikuwa wamepigilia vitu vya namna hii
 Mashabiki walikuwa hawatulii
Mkali wa Bongo fleva Ali Kiba  akiimba jukwaani hii wakati wa show maalum ya Washindi wa Kili Music Award iliyofanyika uwanja wa Sokoine 
 Wasichana waliokuwa wakitoa huduma ya tiketi
 Mkali wa Bongo fleva Ali Kiba akiimba na Omy Dimpoz katika wimbo Nai Nai akiimba jukwaani hii wakati wa show maalum ya Washindi wa Kili Music Award iliyofanyika uwanja wa Sokoine.Picha zote na Father Kidevu Blog
Dimpoz kwa Pozi akipitika katikati ya wacheza show wake.
 Msanii AT kutoka Zanzibar akitumbuiza jukwaani na wacheza sho wake wakati wa show maalum ya Washindi wa Kili Music Award  jijini Mbeya katika Uwanja wa Sokoine jana
Back Stage mambo yalikuwa hivi, Toka kushoto ni Ali Kiba, Omy Dimpoz, Ben Pol na Meneja wa Omy Dimpoz Mubenga. Picha zote na Father Kidevu Blog

***********************
Na  Father Kidevu Blog, Mbeya.
MANENO ya Injili yanayosema Wamwisho anakuwa wakwanza na wakwanza akawa wamwisho yametima hii leo katika Uwanja wa Sokoine Mjini Mbeya pale mkali wa Hip Hop,  Roma  Mkatoliki alipoongoza jahazi la wakali wa Tuzo za Kili Musc Award 2012 katika onesho lao la Uwanjka wa Sokoine mjini Mbeya jana.

Roma akipanda juukwaani akisindikizwa na DJ maarufu DJ Choka, alishangiliwa vilivyo na umati wa watu uliofurika uwanjani hapo pale tu ilipofika zamu yake kupanda jukwaani.

Roma! Roma! Roma! Roma!....hayo ndio yalikuwa maneno ya shwangwe kutoka kwa wapenzi wa burudani kutoka Jijini Mbeya waliofurika katika Uwanja wa Sokonine mjini hapa kushuhudia show hiyo kali ya Washindi wa Tuzo za Kili Music Award 2012.

Roma baada ya kumaliza kuimba nyimbo zake kaza aliwashukuru wana Mbeya kwa kura zao zilizompa ushindi na kuwaambia sasa anamaliza show hiyo ambayo hadi hapo alipofikia alisema wametumia Sh 200/= pekee kati ya Sh 2,000 ya kiingilia waliyotoa.

“Sasa ndugu zangu, nawaambia ukweli hadi sasa mmesha tumia sh 200 tu ya kiingilio chezu,..sasa nawapa show ya Sh 1,800 iliyobaki,” alijigamba Roma ambaye muda wote alikuwa akishangilia na ndipo alipomaliza kwa kuimba Wimbo wa Mathematic uliompa tuzo.

Wasanii wengine waliopanda jukwaani hii leo ni pamoja na Ben Pol, AT, Ali Kiba , Barnaba, Omy Dimpoz  na Suma Lee nao wamefunika vibaya katika Tamasha la Kili Music Award Winners Tour lililofanyika katika Uwanja wa sokoine Mjini Mbeya.

Alianza jukwaani kupanda mshindi wa Tuzo ya wimbo Bora wa R&B.
Msanii Ben Paul ambaye alijinyakulia tuzo hiyo kupitia kibao Number One ambapo nae alishambulia jukwaa na kuwaamsha watu kuwa sasa show imeanza.

Alifuata jukwaani Suma Lee ambaye aliongozwa na show kali kutoka kwa vijana wake wane wakike na wakiume na kushangiliwa vilivyo kwa mkongwe huyo wa Bongo Fleva.

Baada ya Ben Pol, alipanda mkali kutoka Zanzibar ambaye ni mshindi wa Tuzo Wimbo Bora wenye Vionjo vya Kiasili AT na kutoa burudani ya nguvu na  wimbo wa  Vifuu Utundu amabao ulimpa tuzo aliucheza vilivyo na wanenguaji wake wawili wa kike.

Ika fika zamu ya Omy Dimpoz jukwaani kwa kuimba nyimbo yake mpya aambayo alitaraji kuizindua jana katika Ukumbi wa Club Bilicanas jijini Dar es Salaam, single ya Baadae kasha  ile iliyo mpa tuzo ya Wimbo bora wa Kushirikishwa ya Nai Nai aliyo anza kuimba pekeyake na baade kuurudia wimbo huo akiwa na Ali Kiba.

Ali Kiba alibaki jukwaani hapo kama ilivyokuwa mjini Moshi na vijana wake kumfuata kutoa shukrani zao za kupata kura zilizo wapa ushindi wa tuzo ya Wimbo bora wa Zouk Rhumba kupitia wimbo wa Dushelele.

Wakati mara zote pazia la utoaji burudani kwa washindi hao wa tuzo za Kili Music Award 2012 wanaofanya ziara limekuwa likifunga na Roma Mkatoliki leo akapnda wapili kutoka mwisho.

Roma ambaye ni Mshindi wa tuzo mbili za Wimbo Bora wa Hip Hop kupitia wimbo wake wa Mathematics na Tuzo ya Msanii bora wa Hip Hop, alishambulia jukwaa huku viitikio vyake vikiimbwa na DJ Choka na hata alipomaliza show yake bado mashabiki walimtaka aendelee.

Mshindi wa Tuzo ya Mwimbaji bora wa Kiume, Barnaba ndiye aliyefunga pazia hilo kwa siku ya leo mjini Mbeya kwa kuimba  ikiwapo inayovuma kwa sasa ya Magube Gube.

Wasanii hao wiki ijayo wanataraji kutoa burudani kama hiyo jijini Mjini Mtwara na tayari walisha tumbuiza na kuwashukuru mashabiki wao wa Mkoani Dodoma na Jijini Mwanza na Moshi.

Saturday, May 19, 2012

WAKAZI WAILALAMIKIA SERIKALI KUTOKANA NA KUSHINDWA KUDHIBITI VITENDO VYA UPIGAJI NONDO MKOANI MBEYA.




Bwana Oscar
Mbalamwezi (47) mkazi wa mtaa wa Chemchemi Kata ya Igawilo jijini
Mbeya aliyepigwa nondo majira ya saa saba usiku wakati akitoka
kuangalia mpira jana, akiwa amelazwa katika Hospitali ya Rufaa iliyopo
jijini hapa.(Picha na maktaba ya mtandao huu)
******
Habari na Yohana Katema, Mbeya.
Wakazi wa Kata ya Iyela Jijini Mbeya wameulalamikia uongozi wa Serikali ya mtaa, halmashauri na jeshi la polisi kushindwa kudhibiti vitendo vya upigaji nondo pamoja na kuboresha miundombinu ya elimu na barabara.

Baadhi ya wakazi wa kata hiyo Lusekelo Mwalukasa, Ipyana Malangalila na Yusuph Mwakafilwa wamesema mara kwa mara wamekuwa wakitoa malalamiko ya ujenzi wa barabara, vyumba vya madarasa vya shule ya sekondari ya kata pasipo mafanikio ya aina yoyote.

Aidha wamesema licha ya zaidi ya watu 6 kupingwa nondo katika kipindi kifupi hakuna jitihada zozote ambazo wameziona zikichukuliwa na uongozi wa kata katika kuwapata wahusika wa natukio hayo.

Kwa upande wake Afisa mtendaji wa Kata hiyo Ezekiel Kipako, amesema suala la uboreshaji wa barabara linaendelea, ambapo barabara yenye urefu wa kilometa moja na nusu itajengwa kwa kiwango cha lami na suala la upigaji nondo upelelezi unaendelea ili kuwabaini wahusika wa watukio hayo.

Wafanyakazi wa Jiji Waweka Michoro ya Bara barani Jijini Mbeya Leo jioni

 Hizi ni alama zilizo wekwa wakati wanaendelea na kuchora 
 Mmoja ya wafanyakazi akiwa anaendelea kuweka alama za Bara barani

 Baadhi ya Michoro ikiwa imemalizika

Baadhi ya wafanya kazi wakiwa wanapumzika 

Friday, May 18, 2012

USIKU HUU: WATOTO WAZAGAA MTAANI MAENEO YA SOKO MATOKA KUDAKA SENENE

 WATOTO WAKIWA WAMEZAGAA PEMBEZONI MWA BARABARA USIKU HUU KUKAMATA SENENE
 WENGINE WAKIWA KATIKA MITARO NA PEMBENI KWA TAA WAKIKAMATA SENENE 
HAPA WATOTO WAPO MITAA WANAHANGAIKA NA SENENE 

SEMINA YA SIKU YA MAWASILIANO NA HABARI JAMII DUNIANI YAFANA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA MANYUNYU MKOANI NJOMBE

 Viongozi wa TCRA ,Walimu na wanafunzi wakielekea ukumbini katika sherehe hizo 

Wadau Mbali mbali wakisikiliza wakati Semina hiyo inaendelea jana
Kaimu Meneja wa mawasiliano Kanda Ndugu Asajile akiwafundisha wanafunzi umuhimu wa vifaa mbali mbali vya Digital
 Wanafunzi wa Shule ya Manyunyu Mkoani Njombe wakimsikiliza kwa makini Mgeni Rasmi 

 Wanafunzi wa Shule ya Manyunyu Mkoani Njombe wakionesha vipaji vyao katika sherehe hizo 


 Shule ya Sekondari ya wasichana Manyunyu wakikabidhiwa Tv ya kisasa yenye inch 32 LCD


Baadhi ya zawadi walizo kabithiwa shule ya wasichana ya Manyunyu Mkoani Njombe 

Mgeni Rasmi akimkabidhi zawadi mwanafunzi aliye jibu maswali vizuri Hidaya Mapunda aliyepata Laptop ya kisasa 

 Mwanafunzi Hidaya Mapunda akiwaonesha wenzake Laptop yake 
 Mgeni Rasmi katika Sherehe hizo akiendelea kukabidhi zawadi mbali mbali Shuleni hapo 
 Wanafunzi walio Hudhuria katika Sherehe hizo za Siku ya mawasiliano 
 Mgeni Rasmi akipanda Mti shuleni hapo mara baada ya kumaliza shughuli zote 

Habari kamili itawajia siku ya Sherehe zenyewe 
Picha zote na Joseph Mwaisango wa Mbeya yetu Blog